Tani 40,000 za Mbolea zasambazwa kwa Wakulima wa Arusha, Manyara na Kilimanjaro
Maonesho ya 29 ya kilimo kuelekea Sikukuu ya Nanenane 2023 kwa kanda ya Kaskazini yanafanyika katika viwanja vya Nane-Nane, eneo la Njiro, kusini mwa jiji la Arusha, na yamezinduliwa rasmi na Spika wa Baraza la wawakilishi, Zanzibar Zuberi Ally Maulid.